Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mexico yawaonya raia wake US baada mwanamke kufurushwa
Serikali ya Mexico imewataka raia wake wanaoishi Marekani kuchukua tahadhari zaidi mbali na kuwasiliana kwa karibu na ubalozi wao kutokana na kauli za utawala mpya wa Bw. Trump kwamba watafurushwa kutoka Marekani.
Kauli hiyo inakuja baada ya kufurushwa kutoka Marekani kwa mwanamke mmoja raia wa Mexico Guadalupe Garcia de Rayos hapo juzi .
Bi Guadalupe Garcia alikuwa amekwendwa kwa huduma za kawaida katika ofisi ya uhamiaji ya Marekani lakini badala yake akafurushwa kutoka nchini humo.
Sasa serikali ya Mexico inasema hii ni dhahiri kuwa raia wake watakabiliwa na masharti magumu ya kuingia na kuishi Marekani - hivyo kuwashauri wawe na mpango wa dharura ili kuwasaidia iwapo itawalazimu kuihama Marekani kwa haraka .