Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wasichana wenye sura mbaya watakiwa kulipa mahari zaidi India
Kitabu kimoja cha shule katika jimbo la Maharashtra nchini India, kimezua ghadhabu baada ya kusema kuwa watu wenye sura mbaya wanastahili kulipa mahari zaidi.
Kitabu hicho kinasema kuwa ikiwa msichana ana sura mbaya au ni mlemavu, inakuwa vigumu kwa wasichana kama hao kuolewa na hivyo bwana harusi na familia yake huomba mahari zaidi.
Waziri mmoja alivyambia vyombo vya habari kuwa aya hiyo itaondolewa.
Picha za ujumbe huo zilisambazwa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii.
Ulipaji mahari na tamaduni ya karne nyingi kusini mwa bara Asia, ambapo wazazi wa bibi harusi hutoa pesa, nguo na vito vya thamania kwa familia ya bwana harusi.
Mizozo inaweza kuibuka kuhusu no pesa ngapi zinaweza kulipwa. Wakati mwingine wakati bwana harusi na familia yake hawalipwi, Bi harusi anaweza kudhulumiwa vibaya.