Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Upinzani ''wapata ushindi wa mapema'' Gambia
Matokeo ya kwanza kutoka uchaguzi wa urais nchini Gambia yanampa mgombea wa upanzani Adama Barrow ushindi dhidi ya Rais Yahya Jammeh.
Mwandishi wa BBC nchini Gambia anasema amepata thibitisho kuwa bwana Barrow ameshinda kwenye mji mku Banjul.
Hata hivyo ni chini ya asilimia 15 ya karibu wapiga kura 890,000 waliosajiliwa ndio imehesabiwa.
Wanajeshi na polisi hii leo wameweka vituo vya ukaguzi kwenye barabara zinazoingia na kutoka mji mkuu.
Serikali ilizima huduma za mitandao na kufunga simu za kimataifa wakati uchaguzi ulikuwa ukiendelea.