Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kambi ya jeshi la Marekani yashambuliwa Afghanistan
Kumeripotiwa shambulizi kubwa lililofanywa na wanamgambo kwenye kambi kubwa zaidi ya wanajeshi wa Marekani ya Bagram nchini Afghanistan.
Jeshi linaloongozwa na NATO, lilisema kuwa watu wanne waliuawa na hadi 14 kuejruhiwa wakati kifaa kimoja kililipuliwa.
Maafisa wanasema kwa huenda mlipuaji alikuwa ni mshambuliaji wa kujitoa mhanga, ambaye alidanganya kuwa mfanyakazi wakati wafanyakazi walikuwa wakiwasili katika kambi hiyo kwa shughuli za siku.
Kundi la Taliban linasema kuwa ndilo lilihusika. Hakuna taarifa zaidi kuhusu uraia wa wale waliouawa.