Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ntaganda adaiwa kuwafunza mashahidi wake
Waendesha mashtaka katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita wamemshutumu kiongozi wa waasi nchini Congo kwa kuwaingilia mashihidi katika jaribio la kushawishi matokeo ya kesi yake.
Wamesema kuwa uchunguzi uliofanywa katika simu ya Bosco Ntaganda unaonyesha kwamba alikuwa akiwafunza mashahidi wake mbali na kuzuia uchunguzi wa upande wa mashtaka.
Ntaganda aliyepewa jina la utani kama 'The Terminator' amekana mashtaka 18 yanayomkabili ikiwemo mauaji,ubakaji na kuwatumia wanajeshi watoto.
Kiongozi wa mashtaka Fatou Bensouda ametoa wito wa hatua kali kuchukuliwa ili kulinda uadilifu wa kesi hiyo.