Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Amnesty: Polisi wanakiuka haki za binadamu Iraq
Kundi la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa serikali ya Iraq kuchunguza ripoti juu ya polisi kuwatesa na kuwaua raia katika vijiji Kusini mwa Mosul.
Kikundi cha watafiti walikwenda katika eneo hilo baada ya vikosi vya Iraq kufukuza wanamgambo wa Islamic state mwishoni mwa mwezi uliopita.
Mashahidi walisema kuwa takribani watu sita wamepigwa risasi na watu waliovalia sare za polisi. . Mwakilishi Amnesty huko Beirut, Lynn Maalouf, amesema kuwa yeyote anaetuhumiwa kufanya uhalifu wa kivita lazima aadhibiwe, wakisubiri uchunguzi wa kimahakama.