Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Operesheni ya kuukomboa mji wa Raqqa yaanza
Wapiganaji wanaosaidiwa na Marekani, kaskazini mwa Syria, wametangaza wanaanza operesheni ya kuukomboa mji wa Raqqa, shina la Islamic State nchini humo.
Wapiganaji hao ni wa kundi linalojiita wapiganaji wa demokrasi wa Syria, na watasaidiwa na ndege za kijeshi za Marekani.
SDF ni mkusanyiko Waarabu lakini wengi wao ni wapiganaji wa Kikurd.
Na wadadisi wanasema hilo linaweza kuwa tatizo.
Inadaiwa kuwa siku za nyuma, Wakurd waliwafukuza Waarabu kutoka miji fulani, na Wakurd wakisonga mbele hawatokaribishwa katika eneo la Raqqa , ambako watu wengi ni Waarabu.