Kwa picha: Maisha ya Mfalme Bhumibol Adulyadej

Mfalme Bhumibol Adulyadej wa Thailand ndio kiongozi aliyehudumu kwa muda mrefu katika kiti cha ufalme anayeonekana kuwa na ushawishi ulio imarika katika nchi ambayo imeshuhudia mapinduzi kadhaa, katiba 17 na mawaziri wakuu wengi.

Mwanamfalme Bhumibol (kushoto) sasa Mfalme Bhumibol Adulyadej na kakake Mwanamfalme Ananda, aliyekuwa mfalme Ananada Mahidol, shuleni Lausanne Switzerland,mnamo Machi 1935

Chanzo cha picha, AP

Mfalme Bhumibol Adulyadej (kushoto) alipokea madaraka Juni 9 1946 baada ya kakake, Mflame Ananda Mahidol (kulia), kufariki katika ajali iliotokea wakati wa ufyetuaji risasi katika kasri kuu Bangkok. Wanaonekana katika picha hii mnamo 1935 wakiwa shuleni Lausanne, Uswizi.

Mflame Bhumibol Adulyadej na mchumba wake, mwanamfalme Sirikit Lausanne Uswizi Septemba 1949

Chanzo cha picha, AP

Mfalme Bhumibol Adulyadej alizaliwa Cambridge, Massachusetts, ambako babake alikuwa anasoma, na baadaye alisomea Uswizi. Alikutana na mkewe Mwanamfalme Sirikit, akiwa Ulaya.

Familai ya kifalme Thailand katika kasri la Chitralda Bangkok 1955

Chanzo cha picha, AP

Wanandoa hao walizaa watoto 4, lakini wanaonekana hapa 1955 na Mwanamfalme Vajiralongkorn na Ubol Ratana. Hadhi ya ufalme huo ilishuka tangu kuondolewa kwa utawala wa kifalme 1932 na baada ya kuachia madaraka Mfalme Prajadhipok, mjombake Mfalme Bhumibol mnamo 1935.

Rais Dwight Eisenhower na Mfalme Bhumibol na mkewe 1960

Chanzo cha picha, AP

Mfalme Bhumibol alijenga upya hadhi ya Ufalme kupitia ziara kadhaa katika majimbo, kupitia miradi tofuati yaliodhihirisha wasiwasi wake wa muda mrefu kuhusu maendeleo ya kilimo. Alionekana pia na viongozi wa dunia, hapa na rais wa Marekani Dwight Eisenhower alipokuwa katika ziara Washington.

Mfalme Bhumibol na Malkia wa Uingereza, 1960

Chanzo cha picha, PA

Na hapa na Malkia Elizabeth London 1960.

Malkia Elizabeth II na Mfalme Bhumibol Thailand, 1972

Chanzo cha picha, AP

1972 Malkia naye aliizuru Thailand kwa siku tano.

Adulyadej Bhumibol,

Chanzo cha picha, AP

Mfalme Bhumibol aliingilia kati kwa mara ya kwanza mzozo wa kisiasa Thailand mnamo 1973, wakati waandamanaji wanaounga demokrasia mkono walipo shambuliwa kwa risasi na wanajeshi, na waliruhusiwa kujificha kwenye kasri, hatua iliosababisha kuanguka utawala wa aliyekuwa waziri mkuu Jenerali Thanom Kittikachorn.

King Bhumibol azungumza na Jenerali Prem Tinsulanonda 1981

Chanzo cha picha, AP

1981, Mfalme Bhumibol aliingilia kati mzozo wa kisiasa na kupinga wanajeshi waliompindua waziri mkuu na ambaye ni rafiki wa karibu wa Mfalme, Jenerali Prem Tinsulanond (kushoto). Vikosi vinavyoutii ufalme vilidhibiti upya Bangkok.

Mfalme Bhumibol Adulyadej (kulia) na mwanawe mwanamfalme Vajiralongkorn (kushoto)

Chanzo cha picha, AP

Mfalme Bhumibol alifurahia mambo tofauti ikiwemo upigaji picha, kucheza na kutunga nyimbo, kupuliza saxafoni, kuchora na kuandika. Hapa anapuliza saxafoni na mwanawe Mwana mfalme Vajiralongkorn, na wanamuziki wengine. Anafurahia kucheza jazz na wasanii wengine kama Benny Goodman, Stan Getz, Lionel Hampton na Benny Carter.

Mfalme Bhumibol Adulyadej akijitayarisha kutoa haotuba huko Sanam Luang Bangkok, 1996

Chanzo cha picha, AP

Wakati wa mzozo uliozuka dhidi ya aliyekuwa waziri mkuu Thaksin Shinawatra mnamo 2006, Mfalme aliombwa mara kadhaa kuingilia kati hali, lakini alisistiza kuwa haitokuwa sawa.

Raia wanawasha mishumaa nje ya kasri

Chanzo cha picha, AP

Mwaka mmoja baadaye Desemba 5 2007, taifa liliadhimisha miaka 80 ya mfalme Bhumibol.

Mfalme Bhumibol Adulyadej

Chanzo cha picha, AP