Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Waumini wasusia misa ya papa Georgia
Papa Francis ambaye anafanya ziara yake nchini Georgia ameongoza ibada ya misa ambayo ilihudhuriwa na watu wachache mno, baada ya viongozi wa kanisa la Orthodox kuwataka waumini wao kutoshiriki katika ibada ya wakatoliki.
Ujumbe kutoka kanisa hilo la Orthodox ulitarajiwa kuhudhuria ibada hiyo, japo hawakuhudhuria.
Wakati papa francis aliwasili nchini Georgia alilakiwa na waandamanaji wachache wa kanisa la Orthodox, waliokuwa wakiituhumu Vatican kuwa mnyanyasaji wa kidini.