Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mabilioni ya fedha yafujwa Vyuo vikuu Tanzania
Baada ya uhakiki wa miezi kadhaa kwenye vyuo vikuu nchini Tanzania taarifa mpya imeibainisha ufisadi mkubwa ndani ya vyuo vikuu ambapo mabilioni ya fedha za kitanzania zimepotea na kufujwa kwa malipo ya mikopo hewa ya maelfu ya wanafunzi ambao hawapo vyuoni.
Kufuatia ufisadi huo Serikali ya Tanzania sasa imetoa siku saba kwa vyuo vikuu vyote nchini humo vilivyopokea fedha za mikopo kwa wanafunzi hewa ambao hawapo vyuoni kuzirejesha serikalini mara moja.
Aidha pia imevipa agizo vyombo vya dola nchini humo kuanza mara moja kuwachukulia hatua za kisheria wote watakaobainika kuhusika na sakata hilo.