Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wajumbe wa kamati maalum ya madini Tanzania wateuliwa
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, leo Jumatatu ameteua kamati maalum ya pili, itakayofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye mchanga, ndani ya makasha yaliyoko katika maeneo mbalimbali nchini humo.
Kamati hiyo inajumuisha wanauchumi pamoja na wanasheria wa kamati ya kwanza iliyoundwa na wataalamu wa masuala ya Jiolojia, Kemikali na uchambuzi wa kisayansi.
Hayo ni kwa mjibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Wajumbe hao wanane walioko kwenye orodha hiyo, wataapishwa kesho Jumanne asubuhi katika Ikulu ya Rais Jijini Dar es Salaam.