Mahrez, Mane, Salah wawania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2019

Salah

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mohamed Salah

Shirikisho la Soka barani Afrika (Caf) watatoa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2019, leo Jumanne katika sherehe zitakazofanyika nchini Misri katika eneo la ufukwe la Hurghada.

Nyota wa Algeria na Manchester City Riyad Mahrez atakuwa akichuana na nyota wengine wawili wa Liverpool Sadio Mane wa Senegal na Mohamed Salah kutoka Misri.

Mane na Salah waliisadia klabu yao ya Liverpool kutwaa ubingwa wa Ulaya na kombe la dunia la vilabu.

Mahrez aliiongoza Algeria akiwa nahodha katika michuano ya kombe la mataifa ya Africa yaliyofanyika mwaka jana nchini Misri.

Hatua ya mwisho ya upigaji kura kwa tuzo za wanaume na wanawake,watachaguliwa na makocha wakuu/ Wakurugenzi wa ufundi na manahodha wa timu za taifa.

Mane

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Sadio Mane

Wachezaji wa kiume wanawania tuzo

Mohamed Salah (Egypt & Liverpool)

Riyad Mahrez (Algeria & Manchester City)

Sadio Mane (Senegal & Liverpool)

Wanaowania kwa upande wa wanawake

Ajara Nchout (Cameroon & Valerenga)

Asisat Oshoala (Nigeria & Barcelona)

Thembi Kgatlana (South Africa & Beijing Phoenix FC)

Unaweza kusoma

Mahrez

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Mchezaji wa timu ya taifa ya Algeria na klabu ya Manchester City

Mchezaji kijana

Achraf Hakimi (Morocco & Borussia Dortmund)

Samuel Chukwueze (Nigeria & Villarreal)

Victor Osimhen (Nigeria & Lille)

Kocha bora wa mwaka

Aliou Cisse (Senegal - Senegal)

Djamel Belmadi (Algeria - Algeria)

Moïne Chaâbani (Tunisia - Esperance)