Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Ramaphosa anakabiliwa na ushindani mkali wa uongozi wa ANC

Rais wa Afrika Kusini anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Waziri wa zamani wa Afya Zweli Mkhize kuongoza chama.

Moja kwa moja

  1. Kombe la Dunia: Argentina waifunga Ufaransa kwa mikwaju ya penati katika fainali ya kusisimua

    Lionel Messi ameiongoza Argentina kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia baada ya kuifunga Ufaransa kwa mikwaju ya penalti katika mechi ya kusisimua katika historia ya michuano hiyo.

    Argentina walionekana kupoteza kombe hilo, baada ya Kylian Mbappe kufunga mabao mawili katika dakika 10 za mwisho na kupelekea sare katika dakika za nyongeza, baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Messi na Angel di Maria kuwafanya Waargentina hao kuwa mbele kwa mabao 2-0 katika mchezo kipindi chakwanza.

    Messi alirejesha uongozi wao katika kipindi cha nyongeza, kabla ya Mbappe kuwashangaza Wamarekani Kusini tena kwa mkwaju wa penalti na kujipatia hat-trick ya kwanza katika fainali ya Kombe la Dunia tangu 1966.

    Lakini kipa wa Argentina Emiliano Martinez aliokoa penati ya Kingsley Coman na Aurelien Tchouameni kisha akakosa bao, na kumruhusu Gonzalo Montiel kufunga bao la ushindi na kuzua matukio ya ajabu.

    Messi aliyebubujikwa na machozi afikia kilele cha maisha yake katika mchezo wa soka.

    Atakumbukwa daima kwa kuandikisha historia baada ya kufunga bao lake la saba kwenye Kombe la Dunia la 2022, mabao mengi zaidi kwa mchezaji yeyote wa Argentina kwenye mashindano hayo, akimpita Mario Kempes mnamo 1978 (mabao sita).

    Soma:

  2. Furaha na uchungu ulioletwa na kusawazisha kwa Ufaransa

    Argentina 2-2 France

  3. Argentina vs France: Messi na Di Maria waiweka Argentina kifua mbele

    Kipindi cha kwanza kimekamilika na Argentina wanaongoza kwa mabao 2-0.

    Imekuwa mechi ya kushtua ya upande mmoja huku Argentina wakichukua udhibiti kamili.

  4. Ramaphosa anakabiliwa na ushindani mkali wa uongozi wa ANC

    Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anakabiliwa na kinyang'anyiro kikali cha uongozi wa chama dhidi ya waziri wake wa zamani wa afya - ambaye alimlazimisha kujiuzulu kutokana na tuhuma za rushwa.

    Zweli Mkhize anafurahia kuongezeka kwa uungwaji mkono wake kuongezeka dakika za mwisho katika mkutano mkuu wa wajumbe wa chama cha African National Congress mjini Johannesburg, ripoti zinasema.

    Wagombea hao wanapigania kuungwa mkono na wajumbe wapatao 4,426. Mshindi atakiongoza chama kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2024.

    Ikiwa Bw Mkhize atashinda atakuwa kiongozi wa ANC, lakini Bw Ramaphosa atasalia kuwa rais.

    Bw Ramaphosa amekuwa akikabiliwana wito wa kujiuzulu kabla ya kongamano hilo kutokana na madai ya kuficha wizi wa kiasi kikubwa cha fedha za kigeni ambazo zilikuwa zimefichwa kwenye sofa katika shamba lake la kibinafsi.

    Ripoti huru iliyoidhinishwa na spika wa bunge ilisema huenda Bw Ramaphosa alivunja sheria lakini amekana kufanya makosa yoyote.

    Siku ya Jumanne, wabunge wa ANC waliagizwa kumuunga mkono Bw Ramaphosa na kupiga kura ya kukataa jaribio la kuanza mchakato wa kumuondoa madarakani.

    Ni wachache tu waliokaidi amri wakiondoa kikwazo kikubwa ambacho kingemfungia nje ya kinyang’anyiro cha uongozi wa chama.

  5. Israel yamfukuza mwanasheria wa Palestina hadi Ufaransa

    Wizara ya mambo ya ndani ya srael imesema kuwa imemfukuza nchini mwanasheria wa haki za binadamu wa Palestina na Ufaransa baada ya kumtuhumu kwa vitisho vya usalama.

    Salah Hammouri, 37, alisindikizwa kwenye ndege kuelekea Ufaransa na polisi mapema Jumapili asubuhi, wizara ilisema.

    Mkaazi huyo wa mwenye kibali cha kudunu cha kuishi mjini Jerusalem, alinyimwa haki yake ya ukaaji baada ya maafisa kumtyhumu kuwa mwanachama wa shirika la kigaidi.

    Bw Hammouri amekanusha madai hayo na mashirika ya kutetea haki yamelaani hatua hiyo.

    Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa pia ilionyesha kusikitishwa na uamuzi huo, na kusema inalaani "uamuzi wa mamlaka ya Israel, kinyume na sheria, kumfukuza Salah Hammouri Ufaransa".

    Lakini katika taarifa yake, wizara ya mambo ya ndani ya Israel ilisema Bw Hammouri "alikuwa na nia ya kufanya mashambulizi ya kigaidi" dhidi ya "raia na Waisraeli mashuhuri".

  6. Argentina v France: Wargentina waomba katika mitaa ya Buenos Aires

    Huko Buenos Aires - ambapo bado ni asubuhi - mashabiki waliovalia fulani zilizoandikwa jina la Messi mgongoni wanasali mitaani kabla ya mechi ya fainali ya Kombe la Dunia ...

    Maelezo zaidi:

  7. Mashindano ya Qatar yamepata 'mafanikio ya ajabu' - Infantino

    Rais wa Shirikisho la Soka Duniani Fifa, Gianni Infantino anasema Kombe la Dunia la Qatar 2022 limekuwa na "mafanikio ya ajabu katika nyanja zote", ikiwa ni pamoja na upangaji wa mashindano katika majira ya baridi...

    Mwanzoni mwa michuano hiyo Bw. Infantino alizishutumu nchi za Magharibi kwa "unafiki" katika ripoti yake kuhusu rekodi ya haki za binadamu ya Qatar.

    Mchuano huo uligubikwa na masuala mengi ikiwa ni pamoja na vifo vya wafanyakazi wahamiaji na haki ya watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

    Mwezi Februari 2021, gazeti la Guardian lilisema wafanyikazi wahamiaji 6,500 kutoka India, Pakistan, Nepal, Bangladesh na Sri Lanka walikufa nchini Qatar tangu iliposhinda zabuni yake ya Kombe la Dunia.

    Idadi hiyo inatokana na takwimu zilizotolewa na balozi za nchi hizo nchini Qatar.

    Hata hivyo, serikali ya Qatar ilisema jumla ilikuwa ya kupotosha, kwa sababu sio vifo vyote vilivyorekodiwa ni vya watu wanaofanya kazi katika miradi inayohusiana na Kombe la Dunia.

  8. Kombe la Dunia 2022: Jinsi umoja wa familia ulivyomsaidia Kylian Mbappe kupata umaarufu

    Macho yote leo yako kwa mchezaji wa soka wa Ufaransa Kylian Mbappe.

    Je atasaidia mabigwa hao wateteziwa Kombe la Dunia kuhifadhi taji hilo ndio swali lililo midomoni mwa watu wanasubiri mechi ya fainali itakayochezwa saa chache zijazo.

    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ataongoza Ufaransa dhidi ya Argentina jioni hii katika uwanja wa Lusail akiwa na nafasi ya kuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kushinda Kombe la Dunia la pili tangu Pele alipofanya hivyo akiwa na umri wa miaka 21 mwaka 1962.

    Ni mmoja wa wafungaji bora katika dimba hilo - akiwa sawa na mpinzani wa wake Lionel Messi - na tayari amefunga mabao tisa katika mechi za Kombe la Dunia, na kumfanya kuwa mfungaji bora wa 15 katika historia ya michuano hiyo.

    Kwa hakika, ni mchezaji mmoja tu wa kiume katika historia ya Ufaransa aliyefunga mabao zaidi ya Kombe la Dunia - Just Fontaine, akiwa na mabao 13, yote mwaka 1958 - huku mshambuliaji huyu mwenye kasi wa Paris St-Germain akitishia kuvunja rekodi zote mbele yake.

    Maelezo zaidi:

  9. Raia milioni sita wa Ukraine wamerejeshewa umeme - Zelensky

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy ametangaza kuwa nchi hiyo imefanikiwa kurejesha huduma za umeme katika miji iliyoathiriwa na mashambulio ya Urusi

    Akizungumza katika hotuba yake ya kila usiku alisema: Jambo kuu leo ​​ni nishati. Takriban watu milioni 6 wa Ukraine waliweza kurudishiwa umeme kwa siku moja.

    Kazi ya ukarabati inaendelea sasa, wanaendelea bila usumbufu baada ya shambulio kigaidi akiashiria uvamizi wa Urusi.

    Zelensky amewataka washirika wa Magharibi kuipa Ukraine mifumo ya ziada ya ulinzi wa anga haraka iwezekanavyo ili kuwalinda watu dhidi ya "ugaidi wa makombora" wa Urusi.

    "Hasa, nitawakumbusha mara kwa mara ... Washirika wapenzi! Tafuta fursa ya kutoa Ukraine kwa ulinzi wa kuaminika wa anga, ngao ya kuaminika ya ulinzi wa anga. Unaweza. Unaweza kutoa ulinzi kwa watu wetu - ulinzi wa asilimia mia moja kutoka kwa hawa Warusi na mashambulio yao ya kigaidi."

  10. Ukraine: Urusi kupeleka wanamuziki vitani ili kuongeza ari ya wanajeshi wake

    Urusi inasema itawapeleka wanamuziki vitani nchini Ukraine katika jitihada za kuongeza ari ya wanajeshi wake.

    Wizara ya ulinzi ilitangaza kuundwa kwa "kikosi cha wabunifu" wiki hii ikisema kuwa kitajumuisha waimbaji na wanamuziki.

    Wizara ya ulinzi ya Uingereza iliangazia kuundwa kwa kikosi hicho katika sasisho la kijasusi siku ya Jumapili.

    Wakati huo huo, Waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu alitembelea wanajeshi walio vitani nchini Ukraine, serikali ilisema.

    Katika taarifa iliyotumwa kwa Telegram, wizara ya ulinzi ilisema Bw Shoigu "alifika karibu na maeneo ya kupelekwa kwa wanajeshi na kuangalia nafasi za juu za vitengo vya Urusi katika eneo la operesheni maalum ya kijeshi".

    Iliongeza kuwa "alizungumza na wanajeshi waliokuwa mstari wa mbele" - lakini BBC haiwezi kuthibitisha ni lini ziara hiyo ilifanyika au ikiwa Bw Shoigu alitembelea Ukraine yenyewe.

    Ziara hiyo iliyoripotiwa inakuja wakati maafisa wa ulinzi wa Uingereza wanasema kwamba ari ya chini ya wanajeshi wa Urusi inaendelea kuwa "hatari kubwa katika jeshi la Urusi".

    Uingereza ilisema kikosi kipya cha wabunifu - ambacho kinafuata kampeni ya hivi majuzi, inayowahimiza umma kutoa vyombo vya muziki kwa wanajeshi - inazingatia matumizi ya kihistoria ya "muziki wa kijeshi na burudani iliyopangwa" ili kuongeza ari.

    Lakini walihoji kama kikosi kipya kingeweza kuwavuruga wanajeshi, ambao kimsingi wamekuwa na wasiwasi kuhusu "viwango vya juu sana vya majeruhi, uongozi mbaya, matatizo ya malipo, ukosefu wa vifaa na risasi, na ukosefu wa ufafanuzi kuhusu malengo ya vita".

  11. Vita vya Ukraine: Putin akutana na majenerali huku makombora ya Urusi yakishambulia miji

    Rais wa Urusi Vladimir Putin amekutana na wakuu wake wa kijeshi siku hiyo ambayo majeshi yake yalifanya msururu wa mashambulio ya makombora dhidi ya miundombinu ya Ukraine.

    Bw Putin alitumia muda mwingi wa siku ya Ijumaa katika makao makuu ya "operesheni maalum ya kijeshi" kujadili hatua inayofuata ya Urusi nchini Ukraine.

    Haya yanajiri huku baadhi ya maafisa wa jeshi la Ukraine wakidai kuwa Urusi ilikuwa inapanga mashambulizi, labda mapema mwaka ujao.

    Mashambulizi ya Urusi kwenye gridi ya umeme ya Ukraine yamewatumbukiza mamilioni gizani.

    Kanda za mkutano wa Ijumaa zilionyesha Bw Putin akiwa na Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu na Mkuu wa Majeshi Valeriy Gerasimov.

    "Tutawasikiliza makamanda katika kila mwelekeo wa utendaji kazi, na ningependa kusikia mapendekezo yenu kuhusu hatua zetu za haraka na za kati," kiongozi wa Kremlin alionekana akiwaambia maafisa wa kijeshi kwenye TV ya serikali.

    Kuwepo kwa Jenerali Gerasimov kunahitimisha uvumi unaoenea mtandaoni kwamba amefukuzwa kazi.

    Jenerali huyo mwenye umri wa miaka 67 amekuwa akilengwa na wachambuzi wa hawkish, ambao wamemshutumu kwa kuwa mwangalifu sana. Jenerali wa Jeshi la Wanahewa Sergei Surovikin - ambaye aliteuliwa kuwa kamanda wa Urusi nchini Ukraine mnamo Oktoba - pia alikuwepo kwenye mkutano huo, picha zilizotolewa na vyombo vya habari vya serikali zilionyesha.

    Vikosi vya Ukraine vimefanya msururu wa maendeleo makubwa katika miezi ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na kutwaa tena Kherson - jiji kuu pekee lililotekwa na majeshi ya Urusi hadi sasa.

    Na kushindwa kwa vikosi vya Moscow mashariki mwa Ukraine mapema mwaka huu kuliwafanya wakuu wa jeshi kukosolewa na wanahabari wanaounga mkono Kremlin.

  12. Hujambo na karibu.