Mandamano ya saba saba Kenya: Makanisa yatoa wito kwa polisi kijidhibiti
Baraza la Kitaifa la Makanisa nchini (NCCK) limetoa wito kwa idara ya usalama kutotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya Wakenya wakati maandamano ya Saba Saba yanayotarajiwa kufanyika Jumatatu, Julai 7, 2025.
Katika taarifa siku ya Jumapili, NCCK iliibua wasiwasi kuhusu mwenendo unaokua wa kile walichokitaja kama Serikali kuwanyima Wakenya haki ya kuandamana.
Ililalamikia mauaji ya hivi majuzi ya waandamanaji na kauli iliyotolewa Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen ya kuwapiga risasi waandamanaji ikisema inatishia uhuru wa kujieleza nchini Kenya.
Makanisa yanawaomba maafisa wa polisi kutekeleza wajibu wao kwamubu wa Sheria ya Huduma ya Kitaifa ya Polisi na kutoa ulinzi kwa waandamanaji wote.