Papa Leo atoa wito wa 'ujasiri' kumaliza vita vya Ukraine katika hotuba ya Krismasi

Ombi lake linakuja wakati mazungumzo yanayoongozwa na Marekani kuhusu makubaliano ya kusitisha mapigano yakiendelea.

Muhtasari

Moja kwa moja

Asha Juma

  1. Uturuki yawakamata washukiwa 115 wa IS

    Waendesha mashtaka mjini Istanbul wanasema kundi hilo lilikuwa linapanga mashambulizi dhidi ya watu wasiokua Waislamu wiki hii

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Waendesha mashtaka mjini Istanbul wanasema kundi hilo lilikuwa linapanga mashambulizi dhidi ya watu wasiokua Waislamu wiki hii

    Mamlaka nchini Uturuki inasema kuwa imetibua jaribio la mashambulizi yaliyopangwa kufanyika wakati wa sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya baada ya kuwakamata zaidi ya watu 100 wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi linalojiita Islamic State.

    Uvamizi mkubwa ulifanyika katika nyumba 124 kote Istanbul, mwendesha mashtaka mkuu wa jiji hilo alisema, huku bunduki, risasi na "hati za shirika" zikikamatwa.

    Maafisa walisema wafuasi wa IS wamekuwa wakipanga mashambulizi kote Uturuki wiki hii, haswa dhidi ya wasio Waislamu.

    Polisi waliwazuilia washukiwa 115 lakini juhudi zinaendelea kuwatafuta wengine 22, taarifa rasmi ilisoma.

    Ofisi ya mwendesha mashtaka ilisema washukiwa hao walikuwa wakiwasiliana na maafisa wa IS nje ya Uturuki.

    Tangazo hilo linakuja siku mbili baada ya maafisa wa ujasusi wa Uturuki kufanya uvamizi dhidi ya kundi hilo kwenye mpaka wa Afghanistan na Pakistan.

    Raia wa Uturuki ambaye anadaiwa kushikilia wadhifa wa juu katika mrengo wa IS unaohudumu katika eneo hilo alizuiliwa kwa tuhuma za kupanga mashambulizi dhidi ya raia.

    Huduma za usalama za Uturuki mara kwa mara huwalenga watu wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na IS.

  2. Papa Leo atoa wito wa 'ujasiri' wa kumaliza vita vya Ukraine katika hotuba ya Krismasi

    Papa Leo

    Chanzo cha picha, Reuters

    Papa Leo amezitaka Ukraine na Urusi kupata "ujasiri" wa kufanya mazungumzo ya moja kwa moja ili kumaliza vita wakati wa hotuba yake ya kwanza ya Krismasi katika uwanja wa Mtakatifu Petero.

    Alitoa wito wa kukomeshwa kwa mizozo kote dunianii wakati wa hotuba yake ya Urbi et Orbi, ambayo kwa kawaida hutolewa na papa siku ya Krismasi kwa waumini waliokusanyika katika Jiji la Vatican.

    Akiangazia suala la Ukraine, Papa alisema: "Milio ya silaha ikome, na pande husika ziwe na ujasiri wa kushiriki katika mazungumzo ya dhati, ya moja kwa moja."

    Ombi lake linakuja wakati mazungumzo yanayoongozwa na Marekani kuhusu makubaliano ya kusitisha mapigano yakiendelea.

    Marekani imekuwa ikindeleza juhudi za upatanishi kati ya Kyiv na Moscow kwa kujaribu kuweka pamoja makubaliano ya kumaliza mapigano yatayokubaliwa na pande zote mbili, lakini mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo zinazozozana hazijafanyika katika wa duru ya hivi punde ya juhudi za kidiplomasia.

    Wakati wa mahubiri ya mapema ya Siku ya Krismasi katika ukumbi wa St Peter,s Papa Leo aliomboleza hali ya watu wasio na makazi ulimwenguni kote, na uharibifu unaosababishwa na migogoro.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Mapigano makali yazuka katika Mkoa wa Gambella nchini Ethiopia

    Shirika la Madaktari wasiokuwa na mipaka Médecins Sans Frontières (MSF) linasema kuwa limewatibu zaidi ya wagonjwa 100 waliokuwa na na majeraha ya risasi siku ya Jumatano, huku ghasia zikiongezeka katika eneo la Gambela nchini Ethiopia

    Katika taarifa iliyotolewa jana Decemba 24, 2025, MSF ilisema: “ kuongezeka kwa hali ya taharuki katika wiki za hivi karibuni kumesababisha mapigano makali, na kusababisha vifo vingi na kupoteza maisha.

    Vurugu hizi zinaathiri shughuli za kawaida za matibabu, kwani wahudumu wa afya hawawezi kuwafikia wagonjwa.

    Kulingana na Tume ya Haki za Kibinadamu ya Ethiopia, machafuko ya hivi punde-yaliyoangaziwa na risasi katika maeneo kadhaa na kusababisha vifo na majeruhi-yalichochewa na mauaji ya mkuu wa usalama wa mji wa Gambella.

    MSF ilionya kuwa wagonjwa zaidi wanaweza kuwasili ikiwa mapigano yataendelea, ikibaini kuwa tayari ilikuwa imewahudumia takriban majeruhi 50 wiki iliyopita, 19 kati yao wakiwa katika hali mbaya.

    Serikali ya mkoa ilitangaza amri ya kutotoka nje kwa muda usiojulikana kuanzia Jumatano katika maeneo yaliyoathirika na kupiga marufuku ubebaji wa silaha kwa raia, isipokuwa maafisa wa usalama.

  4. Israel yasema italipiza kisasi dhidi ya Hamas kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha vita Gaza

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu amesema kwamba Israeli italipiza kisasi baada ya afisa wa kijeshi kujeruhiwa na mlipuko huko Gaza, huku Hamas ikikanusha kuhusika na kudokeza kwamba kilipuzi kilikuwa kimesalia kutokana na vita.

    Katika hotuba yake katika sherehe ya kuhitimu kwa marubani wa Jeshi la Anga, Netanyahu alitaja tukio hilo huko Rafah, sehemu ya Gaza ambapo vikosi vya Israeli bado vipo na kusema Hamas imeweka wazi kuwa haikuwa na mpango wa kuweka silaha chini kama ilivyotarajiwa chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano ya Oktoba.

    "Israel itajibu ipasavyo," alisema.

    Jeshi la Israeli hapo awali lilisema kwamba kilipuzi kililipuka dhidi ya gari la kijeshi katika eneo la Rafah na kwamba afisa mmoja alijeruhiwa kidogo.

    Hamas ilisema tukio hilo limetokea katika eneo ambalo jeshi la Israeli lilikuwa limedhibiti kikamilifu na kuonya kuwa vilipuzi vilibaki katika eneo hilo na kwingineko tangu vita hivyo, ikisisitiza tena ahadi yake ya kusitisha mapigano ya Oktoba 10.

    Afisa wa Hamas, Mahmoud Merdawi, alisema katika chapisho la awali kwenye mtandao wa X kwamba wapatanishi walikuwa wamearifiwa kuhusu suala hilo.

    Soma zaidi:

  5. Marekani yaamuru jeshi kuzingatia 'karantini' ya mafuta ya Venezuela

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Ikulu ya Marekani imeamuru vikosi vya jeshi lake kuzingatia kutekeleza "karantini" ya mafuta ya Venezuela kwa takriban miezi miwili ijayo, afisa mmoja wa Marekani aliiambia Reuters, akiashiria kuwa Washington kwa sasa ina nia zaidi ya kutumia njia za kiuchumi badala ya kijeshi kuishinikiza Caracas.

    "Ingawa chaguzi za kijeshi bado zipo, lengo ni kwanza kutumia shinikizo la kiuchumi kutekeleza vikwazo ili kufikia matokeo ambayo Ikulu ya White House inayatafuta," afisa huyo alisema Jumatano, akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina.

    Rais Donald Trump amekuwa akionekana hadharani kuwa mwenye haya kuzungumzia malengo yake halisi kuhusu Venezuela, amemshinikiza kwa faragha Rais wa Venezuela Nicolas Maduro kukimbia taifa hilo, Reuters imeripoti.

    Trump alisema Jumatatu itakuwa bora zaidi kwa Maduro kuondoka madarakani.

    "Juhudi hizo hadi sasa zimeweka shinikizo kubwa kwa Maduro, na imani ni kwamba kufikia mwishoni mwa Januari, Venezuela itakuwa inakabiliwa na jinamizi la kiuchumi isipokuwa ikubali kufikia makubaliano makubwa na Marekani," afisa huyo alisema.

    Trump ameishutumu nchi hiyo ya Amerika Kusini kwa kuijazia Marekani dawa za kulevya, na utawala wake kwa miezi kadhaa umekuwa ukishambulia meli za Venezuela zinazotoka Amerika Kusini kwa madai kuwa zimebeba dawa za kulevya.

    Mataifa mengi yameshutumu mashambulizi hayo kama mauaji ya kiholela.

    Soma zaidi:

  6. Algeria yaidhinisha sheria kuwa ukoloni wa Ufaransa ni uhalifu

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Bunge la Algeria limepitisha kwa kauli moja sheria inayotangaza ukoloni wa Ufaransa katika taifa hilo la Afrika Kaskazini kuwa uhalifu, na kudai msamaha na fidia.

    Sheria hiyo pia inaharamisha kutukuza ukoloni, kulingana na ripoti za televisheni ya serikali.

    Kura hiyo ni ishara ya hivi punde ya uhusiano wa kidiplomasia unaozidi kuzorota kati ya nchi hizo mbili, huku baadhi ya waangalizi wakisema uko katika kiwango cha chini kabisa tangu Algeria ipate uhuru miaka 63 iliyopita.

    Ukoloni wa Ufaransa nchini Algeria kati ya mwaka 1830 na 1962 ulighubikwa na mauaji ya halaiki, kufukuzwa kwa watu wengi na kumalizika kwa vita vya umwagaji damu vya uhuru.

    Algeria inasema vita hivyo viliua watu milioni 1.5, huku wanahistoria wa Ufaransa wakisema idadi ya vifo ni ya chini wala sio inayosemwa na Algeria.

    Pia unaweza kusoma:

  7. Wakristo Tanzania wahimizwa kudai haki wakiadhimisha Krismasi

    s

    Chanzo cha picha, Radio Maria

    Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, amesema Watanzania wengi hawashabikii haki na si wadau wa haki, hali inayochangiwa na ujinga, kurubuniwa au kujidai kuwa wadau wa amani bila kuzingatia misingi ya haki.

    Askofu Ruwa’ichi aliyasema hayo wakati wa ibada maalum ya mkesha wa kuadhimisha sikukuu ya Krismasi, ambapo aliwahimiza Wakristo wanaoadhimisha kuzaliwa kwa Mwokozi Yesu Kristo kuwa wadau wa haki katika maisha yao ya kila siku.

    Akifafanua, Askofu Ruwa’ichi alisema Yosefu aliyemkaribisha Yesu nyumbani kwake anatambulika kama mtu wa haki, kwani aliweza kumlinda, kumtunza na kumkaribisha Maria kumlinda na kumtunza.

    "Yosefu aliyemkaribisha Yesu nyumbani kwake anatambulika kama mtu wa haki, aliweza kumkaribisha Maria kumlinda na kumtunza, sisi sote kwa nguvu ya ubatizo wetu ambao umetufunganisha na Kristo Mwokozi tunaitwa tuwe watu wa haki...haki ni ule uelewa wa kutambua mastahili ya wengine na kuyaheshimu".

    Alisisitiza kuwa Wakristo wote, kwa nguvu ya ubatizo wao unaowaunganisha na Kristo Mwokozi, wameitwa kuwa watu wa haki, akieleza kuwa haki ni uelewa wa kutambua mastahili ya wengine na kuyaheshimu ipasavyo.

    Askofu huyo aliwakumbusha waumini kuwa haki ndiyo msingi wa amani ya kweli, akionya kuwa hakuna amani ya kudumu bila haki, hivyo kuwataka Watanzania kuwa wadau wa amani kwa kuanzia kwenye haki.

    Katika mahubiri yake, aliuliza kwa msisitizo akisema, “Ewe mwana wa Dar es Salaam, ewe Mtanzania, je wewe ni mtu wa haki?” akilenga kuwahamasisha waumini kujitathmini binafsi.

    Wakati huo huo, Wakristo kutoka Afrika Mashariki wameungana na wenzao duniani kote kuadhimisha sikukuu ya Krismasi, huku viongozi mbalimbali akiwemo Rais wa Kenya William Ruto na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan wakitoa salaam za heri ya Krismasi kwa waumini.

    Rais Samia Suluhu Hassan aliandika katika mtandao wa kijamii "Ninawatakia kheri ya sikukuu ya Krismasi wakristo wote na watanzania wote Mwenyezi Mungu awabariki nyote".

    Naye rais Ruto alionekana katika video akiwatakia wakenya heri ya sikukuu na kuwaasa kuendesha vyombo vya moto kwa uangalifu kuepuka ajali.Baadhi ya raia waishio katika Maeneo yanayo kabiliana na ukosefu wa usalama nchini Congo DRC, wameelezea kuadhimisha Siku kuu hiyo katika hali ya wasiwasi, huko wakitaka kuimarishwa kwa amani na Usalama nchini humo.

  8. Mlipuko wa bomu katika msikiti uliojaa watu Nigeria waua watu watano

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Msemaji wa polisi amesema watu watano wameuawa katika mlipuko wa bomu katika msikiti uliojaa watu kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno nchini Nigeria.

    Nahum Daso aliambia vyombo vya habari vya ndani kwamba watu wengine 35 walijeruhiwa katika mlipuko huo katika soko la Gamboru la Maiduguri, mji mkuu wa jimbo hilo, wakati wa sala ya jioni.

    Picha ambazo hazijathibitishwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonekana kuonyesha matokeo ya mlipuko huo, huku watu wakiwa wamesimama katika eneo la soko na vumbi likiwa limetanda angani.

    Hakuna kundi lililokiri kutekeleza shambulio hilo, lakini awali wanamgambo walilenga misikiti na maeneo yenye watu wengi katika eneo hilo kwa mashambulizi ya kujitoa mhanga na vifaa vya kulipuka vilivyotengenezwa kwa njia ya kienyeji.

    Pia unaweza kusoma:

  9. Sean 'Diddy' Combs awasilisha rufaa ya kuachiliwa huru mara moja

    .

    Chanzo cha picha, Reuters/Jane Rosenberg

    Sean "Diddy" Combs ameiomba mahakama ya rufaa kumwachilia huru kutoka gerezani na kubatilisha hukumu yake ya makosa mawili yanayohusiana na ukahaba.

    Katika kesi ya mahakama ya kuomba rufaa ya haraka, wakili wa tajiri huyo wa muziki wa rapa alidai kwamba alihukumiwa isivyofaa, na kwamba mwenendo uliosababisha kuhukumiwa kwake haukuwa wa uhalifu wa jinai.

    Wakili Alexandra Shapiro aliita kifungo cha miezi 50 cha Combs jela "kinyume cha sheria, kinyume cha katiba, na upotoshaji wa haki". Aliiomba mahakama ya rufaa kuamuru kwamba Combs ahukumiwe tena, ikiwa jopo litachagua kutotupilia mbali hukumu yake yote.

    Ombi hilo ni jaribio la hivi karibuni la timu yake la kupunguza kifungo chake au kutupilia mbali hukumu yake.

    Soma zaidi:

  10. Watu kumi na mmoja wakamatwa kwa shambulio la ufyatuaji risasi Afrika Kusini

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Washukiwa kumi na mmoja wamekamatwa kuhusiana na shambulio la ufyatuaji risasi watu wengi lililosababisha vifo vya watu tisa katika mgahawa mmoja nchini Afrika Kusini siku ya Jumapili.

    Polisi walianzisha msako mkali kwa watu 12 wasiojulikana waliokuwa wamewafyatulia risasi yapata saa 1:00 za eneno (saa 23:00 GMT Jumamosi) katika eneo la Bekkersdal, karibu na Johannesburg.

    Siku ya Jumatano, naibu kamishna wa polisi wa mkoa, Meja Jenerali Fred Kekana alisema washukiwa tisa waliokamatwa ni raia wa Lesotho, huku mmoja akitoka Msumbiji.

    Mshukiwa mwingine, anayeaminika kuwa mfanyakazi wa migodini kutoka Afrika Kusini, pia alikamatwa.

    Mauaji nchini Afrika Kusini - ambayo ni ya viwango vya juu zaidi duniani - mara nyingi husababishwa na mabishano, wizi na vurugu za magenge.

    Ingawa shambulio hilo lilionekana "bila kuchochewa" wakati huo, uchunguzi wa awali unaonyesha ufyatuaji huo uliokana na vita vya uchimbaji madini kwa njia haramu.

    Wakati wa shambulio hilo, watu wenye silaha waliendelea kufyatua risasi huku watu wakikimbia kwenye baa, na kuwaua wawili pamoja na dereva wa teksi ambaye alikuwa amemshusha abiria mmoja karibu.

    Baada ya kuwakamata, bunduki kadhaa zisizo na leseni ikiwemo bunduki aina ya AK-47, zilipatikana zikiwa mikononi mwa washukiwa.

    Ufyatuaji risasi wa Jumapili ulitokea wiki mbili tu baada ya shambulio jingine katika eneo la Saulsville katika mji mkuu wa Pretoria, ambapo watu kumi na mmoja akiwemo mtoto wa miaka mitatu waliuawa.

    Soma zaidi:

  11. Maafisa wabaini nyaraka zaidi ya milioni moja zinazohusishwa na kesi ya Epstein

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maafisa wa Marekani wamegundua zaidi ya hati milioni moja zaidi zinazoweza kuhusiana na mhalifu wa kingono marehemu Jeffrey Epstein ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na watoto, ambazo wanapanga kuzitoa siku zijazo, maafisa wanasema.

    Mwanasheria wa Marekani wa Wilaya ya Kusini ya New York na FBI wameifahamisha Idara ya Sheria (DoJ) kuhusu ugunduzi huo na kukabidhi hati hizo kwa wanasheria kuzipitia.

    "Tuna wanasheria wanaofanya kazi saa 24 kupitia na kufanya mabadiliko yoyote yanayohitajika kisheria ili kuwalinda waathiriwa, na tutatoa hati hizo haraka iwezekanavyo," Idara ya sheria ilisema kwenye mitandao ya kijamii Jumatano.

    Idara ilisema kwamba kutokana na wingi wa nyenzo, mchakato huo unaweza kuchukua "wiki chache zijazo".

    Taarifa hiyo haikubainisha jinsi waendesha mashtaka wa FBI na New York walivyopata taarifa hizo za ziada.

    Taarifa hizi zinajitokeza baada ya idara ya sheria kutoa maelfu ya hati wiki iliyopita - baadhi zikiwa zimefanyiwa marekebisho sana - zinazohusiana na uchunguzi wao kuhusu Epstein.

    Faili hizo zilitolewa baada ya Bunge kupitisha Sheria ya Uwazi ya Faili za Epstein - iliyosainiwa na Rais wa Marekani Donald Trump - ambayo iliamuru shirika hilo kushirikisha hati zote na umma huku likilinda utambulisho wa waathiriwa.

    Soma zaidi:

  12. Krismasi njema msomaji wetu. Karibu katika matangazo yetu ya leo ikiwa ni tarehe 25/12/2025.