Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Khamenei: Wamarekani wanapaswa kujua kwamba ikiwa wataanzisha vita wakati huu vitakuwa vita vya eneo zima

Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ametahadharisha katika kukabiliana na ongezeko la vikosi vya kijeshi vya Marekani katika eneo hili: "Wamarekani wanapaswa kujua kwamba iwapo wataanzisha vita, mara hii vitakuwa vita vya kieneo."

Muhtasari

Moja kwa moja

Abdalla Seif Dzungu

  1. Israel kupiga marufuku MSF kufanya kazi huko Gaza kwa kukataa kutoa orodha ya wafanyikazi wake

    Israel inasema itapiga marufuku Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) kufanya kazi huko Gaza baada ya shirika la misaada la matibabu kukataa kukabidhi orodha ya wafanyikazi wake katika eneo hilo.

    Serikali ya Israel ilikuwa imeamuru mashirika 37 kuwasilisha nyaraka kuhusu wafanyakazi wao wa ndani na wa kimataifa huko Gaza, wakidai baadhi katika MSF walikuwa na uhusiano na makundi yenye silaha Hamas na Islamic Jihad.

    Shirika la hisani limekanusha vikali hili.

    MSF ilitangaza siku ya Ijumaa kwamba haitashiriki orodha ya wafanyakazi wake wa Palestina na kimataifa na mamlaka ya Israel kwa kuwa haijapata "hakikisho la usalama wa wafanyakazi wetu".

    Katika kujibu, Israel ilisema "inaelekea kusitisha shughuli" za MSF huko Gaza.

    Wizara ya Israel ya Masuala ya Diaspora na Kupambana na Kupinga Uyahudi ilisema uamuzi huo ulifuatia "kushindwa kwa MSF kuwasilisha orodha za wafanyikazi wa ndani, hitaji linalotumika kwa mashirika yote ya kibinadamu yanayofanya kazi katika eneo hilo".

    Mnamo tarehe 30 Disemba, Israel ilitangaza kuwa ingefuta leseni za mashirika 37 ya kimataifa yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi huko Gaza na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa, ikisema kuwa yameshindwa kukidhi mahitaji mapya ya usajili.

  2. Naibu Kamanda wa IRGC: Kuwepo kwa meli za Marekani katika eneo hilo ni operesheni ya kisaikolojia, hatupaswi kuzingatia.

    Naibu kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi alipuuza ongezeko la wanajeshi wa Marekani katika Mashariki ya Kati.

    Ahmad Vahidi amesema kuwasili kwa meli za Marekani katika eneo hilo "ni sehemu ya operesheni za kisaikolojia za adui na hazipaswi kuzingatiwa."

    Bw. Vahidi pia alisema kuwa utayari wa jeshi la Iran uko "katika hali bora" na "kubwa zaidi" kuliko wakati wa vita vya siku 12 na Israeli.

    Naibu kamanda wa IRGC alisema kuwa "maadui wanatafuta kutawala anga ya vita na hii ni sehemu ya shughuli zao za kisaikolojia; hatupaswi kuingia katika mtego huu na shughuli za nchi hazipaswi kuathiriwa na operesheni hizi kwa njia yoyote."

  3. Mkurugenzi wa Melania Brett Ratner aonyeshwa akiwakumbatia wasichana katika picha za Epstein

    Mkurugenzi wa filamu mpya ya Mke wa Rais wa Marekani Melania Trump ameonekana akimkumbatia msichana katika picha zilizotolewa na Idara ya Sheria ya Marekani siku ya Ijumaa.

    Brett Ratner, ambaye pia aliongoza filamu za Rush Hour na X-Men: The Last Stand, anaweza kuonekana akiwa ameketi kwenye sofa kando ya marehemu mhalifu Jeffrey Epstein na wanawake wawili ambao utambulisho wao haujafichwa.

    Wakati picha hizo zilipigwa bado haijulikani, ingawa zinaonekana kuwa zilipigwa katika eneo moja na picha za Ratner na Epstein pamoja na wakala wa wanamitindo wa Ufaransa marehemu Jean-Luc Brunel ambazo zilitolewa Desemba.

    Hakuna dalili ya makosa kutoka kwa faili. BBC imewasiliana na mwakilishi wa Ratner kwa maoni yake.

    Picha hizo mpya zilizotolewa zilikuwa sehemu ya mamilioni ya faili zinazohusiana na mhalifu wa ngono marehemu, ambaye alikufa kizuizini mnamo 2019 akisubiri kesi ya mashtaka ya biashara ya ngono.

    Msururu wa vijipicha vya mkusanyiko wa picha unaonyesha Ratner, Epstein na Brunel wakitabasamu na kustarehe na wanawake tofauti, ambao utambulisho wao wote umefichwa.

    Sheria ambayo ilisababisha kutolewa kwa faili hizo kuamuru zifanyiwe uchunguzi upya ili kulinda waathiriwa au uchunguzi unaoendelea - ingawa wakili anayewakilisha wengi wao amesema utambulisho wa manusura wengi ulifichuliwa .

    Faili hizo zilitolewa siku moja na Melania: 20 Days to History, picha ya nyuma ya pazia kuhusu maisha ya mke wa rais katika siku chache kabla ya kuapishwa kwa mumewe Januari 2025.

  4. Mashambulizi mabaya ya bunduki na mabomu yaliathiri jimbo la Balochistan nchini Pakistan

    Msururu wa mashambulizi ya bunduki na mabomu katika jimbo la kusini-magharibi la Balochistan nchini Pakistan yamesababisha vifo vya raia 31 na maafisa 17 wa usalama, Waziri Mkuu wa eneo hilo Sarfraz Bugti anasema.

    Vikosi vya usalama vilivyokabiliana na ghasia hizo viliwaua washambuliaji wasiopungua 145, kulingana na Bugti.

    Kundi la waasi la Balochistan Liberation Army (BLA) awali lilisema ndilo lililohusika na mashambulizi hayo, likidai makumi ya wanajeshi waliuawa.

    Ongezeko hilo ni moja ya siku mbaya zaidi za ghasia katika jimbo hilo maskini, ambapo serikali ya Pakistan imekuwa ikipambana na uasi wa kikabila kwa miongo kadhaa.

    Pakistan iliishutumu India kwa kuunga mkono BLA. Delhi imekanusha mara kwa mara tuhuma kama hizo.

  5. Iran iko katika 'majadiliano mazito' na Marekani, Trump asema, huku tishio la kijeshi likikaribia

    Rais Trump amethibitisha kuwa Iran iko kwenye "majadiliano mazito" na Marekani kufuatia kuimarika kwa vikosi vya kijeshi vya Marekani katika Ghuba.

    Rais wa Marekani alisema anatumai mazungumzo na Iran yataleta kitu "kinachokubalika", huku mvutano kati ya nchi hizo mbili ukiendelea kuwa juu.

    Afisa mkuu wa usalama wa Iran Ali Larijani pia alisema mfumo wa mazungumzo unaendelea.

    Trump ametishia kuingilia kati Iran kuhusu azma yake ya nyuklia na baada ya ukandamizaji wake mbaya dhidi ya maandamano dhidi ya serikali.

    Iran imesema itajibu "mara moja na kwa nguvu" kwa uchokozi wowote wa nchi kavu au baharini.

    Iran inatarajiwa kuanza mazoezi ya majini ya siku mbili ya moja kwa moja siku ya Jumapili katika Mlango-Bahari wa Hormuz - mojawapo ya njia muhimu zaidi za meli duniani na njia muhimu ya usambazaji wa mafuta.

    Takriban thuluthi moja ya mafuta yanayouzwa duniani hupitia njia hiyo ya baharini, ambayo ina upana wa takriban kilomita 33 (maili 21) katika sehemu yake nyembamba zaidi kati ya Iran na Oman.

    Iran katika siku za nyuma ilitishia kufunga njia hiyo iwapo kutatokea shambulio dhidi yake.

    Marekani imeionya Iran dhidi ya "tabia zisizo salama na zisizo za kitaalamu" karibu na vikosi vyake katika eneo hilo.

    Kama sehemu ya uimarishaji wake wa vikosi Marekani imetuma shehena yake ya ndege USS Abraham Lincoln katika eneo hilo na mwishoni mwa wiki iliyopita kamandi kuu ya Marekani ilisema ilikuwa inafanya kazi katika Bahari ya Arabia.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi alijibu kwa kusema: "Jeshi la Marekani sasa linajaribu kuamuru jinsi Jeshi letu lenye Nguvu linapaswa kufanya mazoezi ya shabaha katika katika himaya yetu."

  6. Mshauri wa usalama wa kitaifa wa Waziri Mkuu wa Slovakia ajiuzulu kwa kuhusishwa na Epstein

    Mshauri wa usalama wa taifa wa waziri mkuu wa Slovakia amejiuzulu baada ya nyaraka zilizotolewa na Marekani kuonyesha alibadilishana ujumbe kuhusu wasichana na diplomasia na mshukiwa wa ngono marehemu Jeffrey Epstein.

    Robert Fico alitangaza kuwa amekubali kuondoka kwa Miroslav Lajčák katika ujumbe wa video siku ya Jumamosi, akielezea mshauri huyo kama "chanzo cha ajabu cha uzoefu katika diplomasia na sera za kigeni".

    Kujiuzulu kunajiri siku moja baada ya faili milioni tatu zinazohusiana na mfadhili huyo mwenye ushawishi mkubwa kutolewa na Idara ya Sheria ya Marekani.

    Ingawa faili hazionyeshi makosa yoyote kwa upande wa walioangaziwa, ikiwa ni pamoja na Lajčák, zimeibua maswali mapya kwa wale waliohusishwa na Epstein.

  7. Khamenei: Ikiwa wataanzisha vita, vitakuwa vita vya kikanda

    Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ametahadharisha katika kukabiliana na ongezeko la vikosi vya kijeshi vya Marekani katika eneo hili: "Wamarekani wanapaswa kujua kwamba iwapo wataanzisha vita, mara hii vitakuwa vita vya kieneo."

    Shirika la Habari la Tasnim limeripoti kuwa kiongozi huyo wa Iran alitoa hotuba kwa kundi la watu leo.

    Bw. Khamenei alisema kwamba "ukweli kwamba nyakati fulani wanazungumza kuhusu vita na kuzungumzia kuhusu ndege na meli na kadhalika si jambo jipya," na "katika siku za nyuma, Wamarekani walitishia mara kwa mara katika hotuba zao na kusema kwamba chaguzi zote ziko mezani, ikiwa ni pamoja na chaguo la vita."

    Akimzungumzia Rais Donald Trump wa Marekani, Kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ameongeza kuwa: "Sasa bwana huyu (Trump) pia anadai mara kwa mara kwamba tulileta meli ya kivita na... taifa la Iran halipaswi kuogopa na mambo haya, wananchi wa Iran hawaathiriwi na vitisho hivyo."

    Bwana Khamenei amesisitiza kuwa, Iran sio inayoanzisha vita na haina nia ya kushambulia nchi yoyote, lakini "taifa la Iran litatoa pigo kali dhidi ya yeyote anayeishambulia na kuinyanyasa."

  8. Wabunge wa Iran waonekana bungeni wakiwa wamevalia sare za Jeshi la Iran IRGC

    Vyombo vya habari vya Iran vimeripoti kuwa hii leo, wabunge wa Iran wamejitokeza bungeni wakiwa wamevalia sare za IRGC kujibu Umoja wa Ulaya kuijumuisha IRGC katika orodha yake ya makundi ya kigaidi, na kutangaza kuiunga mkono taasisi hiyo ya kijeshi.

    Shirika la Habari la Tasnim pia limeripoti kuwa bendera yenye kauli mbiu "IRGC ndio shirika kubwa zaidi la kupambana na ugaidi duniani" pia iliwekwa kwenye jukwaa la kikao cha Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu.

    Wakati wa hotuba kabla ya agizo hilo, wawakilishi hao pia waliimba "Aibu kwa Ulaya." Umoja wa Ulaya ulitangaza Alhamisi, Januari 29, kwamba umeliorodhesha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kama shirika la kigaidi.

    Hatua ya hivi majuzi ya Umoja wa Ulaya imeibua hisia kali kutoka kwa maafisa wengi wa Jamhuri ya Kiislamu.

  9. Iran: Kwa mujibu wa sheria ya kulipiza kisasi, majeshi ya nchi za Ulaya yanachukuliwa kuwa makundi ya kigaidi

    Mohammad Baqer Qalibaf, Spika wa Bunge la Iran amesema katika kikao cha hadhara hii leo: "Kwa mujibu wa kifungu cha 7 cha sheria kuhusu hatua za kukabiliana na tangazo la IRGC kuwa ni shirika la kigaidi, majeshi ya nchi za Ulaya yanahesabiwa kuwa ni makundi ya kigaidi, na matokeo ya hatua hiyo yatakuwa jukumu la Umoja wa Ulaya."

    Bw. Qalibaf alisema: "Wazungu walijipiga risasi miguuni kwa kujaribu kuipiga IRGC, ambayo ilikuwa kikwazo kikubwa cha kuenea kwa ugaidi Ulaya."

    Kulingana na yeye, "hatua ya kutowajibika" ya Umoja wa Ulaya ilikuwa "kufuata maagizo ya Rais wa Marekani" na Israel, ambayo "itaharakisha njia ya Ulaya ya kutokuwa na umuhimu katika utaratibu wa ulimwengu ujao."

    Umoja wa Ulaya ulitangaza Alhamisi, Januari 29, kwamba umeliorodhesha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kama shirika la kigaidi.

    Hatua ya hivi majuzi ya Umoja wa Ulaya imeibua hisia kali kutoka kwa maafisa wengi wa Jamhuri hiyo ya Kiislamu.

  10. Natumai hujambo