Vita vya Ukraine: Fahamu chombo kipya cha propaganda kinachotumiwa na Urusi

Chanzo cha picha, Southern Front
Mji wa Berdyansk ulikuwa umetekwa na wanajeshi wa Urusi chini ya wiki moja, lakini chombo kipya kinachounga mkono-Kremlin mitandaoni kilikuwa tayari kimeingia.
Kampuni hiyo ambayo jina lake linajulikana kama Southern Front, kinaandaa na kusambaza propaganda zinazomuunga mkono-Vladimir Putin kupitia mitandao ya YouTube, app ya mtandao wa kijamii wa Telegram, na kupitia tuvuti ambayo inalenga maeneo mapya yaliyo chini ya udhibiti wa Warusi.
Southern Front iliweka mtandaoni ujumbe wake wa kwanza kuhusu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, na sasa ina waandishi kwadhaa wanaotayarisha habari kila siku.
BBC imegundua kuwa matokeo katika ripoti yake si sawa kama yalivyoonekana mara ya kwanza.
Mapema mwezi Machi, mwandishi wa Southern Front alikuwa kwenye eneo la tukio huko Berdyansk. Waliripoti kwamba wanajeshi wa Urusi walikuwa wamezuia shambulio hilo, na kuwaua wanaume wawili wa Morocco waliohusika. Mwandishi huyo alidai watu hao walikuwa wakifanya kazi kama mamluki wa Ukraine.
Lakini inaonekana vipengele vya video vilivyowekwa vimeigizwa.

Chanzo cha picha, Southern Front
Wanaume wawili wa Morocco waliotambuliwa katika shambulio hilo inadaiwa walikutwa na vibali vyao vya makazi ya Ukraine bado vikiwa juu yao.
BBC ilimsaka mmoja wa watu waliohusishwa. Kulingana na ripoti alikuwa amekufa, lakini tulizungumza naye kwenye mitandao ya kijamii. Aliomba jina lake lisitajwe lakini anasema hakufahamu kuhusu ripoti ya Urusi na kwamba aliondoka Ukraine kabla ya uvamizi huo na kurejea Morocco.
Southern Front huchapisha mara kwa mara video zilizo na madai ambayo hayajathibitishwa.
Ripoti nyingi za kawaida zinadai kuonyesha "maisha ya amani" imeanzishwa katika maeneo yaliyokaliwa, na hutumia masimulizi ya kuhalalisha uvamizi wa Urusi.
Katika kifurushi kimoja cha video, mwandishi anaripoti kutoka maktaba ambapo anasema alipata mifano mingi ya vitabu vyenye "ishara za Nazi". Hakuna ushahidi unaoonekana kwenye skrini. Vitabu vinavyoonekana kwenye kamera vinajumuisha kazi za waandishi wa kisasa wa Ukraine kuhusu matukio ya kweli ya kihistoria, kama vile vita vya Ilovaisk.

Chanzo cha picha, Southern Front
"Southern Front inaweza kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Urusi wa kuanzisha udhibiti wa maeneo yanayokaliwa ya Ukraine," anasema Julia Smirnova, mchambuzi katika Taasisi ya Majadiliano ya Kimkakati.
Kampuni hiyo na idhaa zake za mitandao ya kijamii zinaonyesha uvamizi wa Urusi katika maeneo ya kusini mwa Ukraine kama "ukombozi", na vikosi vya Urusi kama "walinzi", anasema Bi Smirnova.
Southern Front inamilikiwa na nani?
Southern Front iliibuka saa chache baada ya wanajeshi wa Urusi kuvamia tarehe 24 Februari, wakati kituo chake cha Telegram kilichapisha ujumbe wake wa kwanza.
"Vladimir Putin alitangaza kuanza kwa operesheni maalum ya kijeshi na kuondoa Wanazi katika eneo la Ukraine!" iliandikia hadhira ndogo ya waliojisajili 25 (sasa 23,000).

Chanzo cha picha, Southern Front
Tovuti ilisajiliwa siku moja baadaye. Hapo awali kwa kutumia seva ya Kirusi kutoka St Petersburg, kisha ikahamia kwa mtoa huduma wa Marekani Cloudflare, ambayo inaruhusu tovuti kuficha utambulisho wa mmiliki wake.
Idhaa hii hutoa huduma ya habari ya kawaida inayoongozwa na watangazaji wachanga, wanaoonekana kama wasomi kutoka jimbo la Crimea lilijitenga na Ukraine. Vyanzo vya habari vya Ukrane vimekatwa kwa kiasi kikubwa.
Mmoja wa watangazaji aliyewasiliana na BBC idhaa ya Kirusi alisema walifanya kazi bila malipo, na hakujua ni nani aliyefadhili shughuli hizo.
Pia tuliuliza Southern Front kuhusu umiliki, lakini hatukujibu.

Chanzo cha picha, Southern Front
Lakini inaonekana kana kwamba shirika lenye ushawishi na uhusiano na serikali ya Urusi ambayo linahusika katika kutoa maudhui ya Southern Front.
Baada ya kutazama video kadhaa, tuliona baadhi zilirekodiwa katika chumba cha mikutano zikionyesha nembo ya Kamati ya Ushirikiano ya Urusi-Donbas, ambayo inapendekeza kwamba majengo ya shirika hili yanatumiwa kurekodia filamu.
Dhamira ya kamati ya Crimea, iliyoorodheshwa kwenye tovuti yake, ni kujenga uhusiano wa kiuchumi na kibinadamu na Crimea iliyounganishwa na jamhuri za kujitenga zinazounga mkono Urusi katika Donbas.
Viongozi wa maeneo haya yanayojiita jamhuri ya mashariki mwa Ukraine wana majukumu muhimu katika shirika hilo. Mratibu ni Andrei Kozenko - mbunge wa zamani wa Urusi, kwa sasa anakabiliwa na vikwazo vya Marekani na Umoja wa Ulaya.

Chanzo cha picha, Southern Front
Maudhui ya Southern Front yanafika mbali zaidi ya tovuti yake.
Mtandao wa akaunti za Telegraph zenye nia kama hiyo zinazofunika miji inayokaliwa mara nyingi huchapisha nyenzo zake
Kwa pamoja, vituo hivi sasa vina zaidi ya wafuatiliaji 80,000, ingawa utafiti wetu unaonyesha kuwa angalau thuluthi moja ya hizi huenda zililipwa ili kuongeza hadhira kwa njia isiyo halali. Katika chaneli tatu idadi ya wafuasi iliongezekwa kwa zaidi ya 10,000 kwa saa moja usiku wa Machi 29 , kulingana na uchambuzi wa TG Stat, ambao hufuatilia data ya Telegraph.
Licha ya ufuasi mdogo kwenye mitandao ya kijamii, Southern Front imechochewa na akaunti zenye ushawishi mkubwa, ikiwa ni pamoja na mwanablogu mwenye wafuasi zaidi ya 650,000, na vyombo vya habari vinavyounga mkono Kremlin kama vile Moskovsky Komsomolets - gazeti la Moscow linalopatikana katika nchi nyingi za baada ya Soviet. .
Lakini mapambano yameanza. Wiki iliyopita, wanaharakati wanaounga mkono Ukrainian walidukua tovuti ya Southern Front na ujumbe kuhusu Kherson, ambayo watawala wapya wa eneo hilo wanasema wanataka kutwaliwa na Urusi.

Moja ya machapisho hayo yameonya kuwa watu wowote watakaoshiriki katika kile kinachoitwa kura ya maoni kuhusu mustakabali wa eneo hilo wataadhibiwa na Ukraine.
Ilisema: "Karibu Kuzimu!!!"
Licha ya shambulio hilo, tovuti ilianza tena kufanya kazi muda mfupi baadaye.
Kuna dalili za wasiwasi kwa wenyeji ikiwa mradi mwingine utajianzishwa. Baada ya Crimea iliyo karibu kunyakuliwa mwaka wa 2014, vyombo huru vya habari vilifukuzwa, anasema Bi Smirnova.
"Kusini mwa Ukraine, mamlaka za Urusi zina uwezekano wa kufuata njia sawa kwa kutishia na kuwakamata waandishi wa habari huru, kunyamazisha vyombo huru vya habari na kuweka njia za propaganda badala yake."












