Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ongezeko la bei ya mkate lazua maandamano Sudan
Kumekuwa na maandamano katika miji mbalimbali nchini Sudan baada ya bei ya mkate kupanda maradufu.
Hatua hiyo ya maandamano imekuja baada ya serikali ya nchi hiyo kufanya maamuzi ya kuondoa ruzuku ya vyakula na kusababisha gharama ya mkate kuwa kubwa mara dufu.
Huko magharibi mwa Darfur, mwanafunzi mmoja aliyekuwa katika maandamano aliuwawa na wengine sita kujeruhiwa mara baada ya maandamano hayo kugeuka kuwa ya fujo.
Katika mji mkuu wa Khartoum, polisi walitumia mabomu ya machozi kusambaratisha watu ambao walikuwa wamefunga barabara na kuchoma matairi.
Naibu waziri wa mambo ya ndani alikanusha kuwa maandamano hayo hayakutoea kutokana na ongezeko la bei na kuahidi kuwa atawashughulikia wale wote waliokuwa wanafanya maandamano yenye fujo.
Serikali ya Sudan pia imezuia magazeti yote yaliyokosoa ongezeko la bei kutouzwa.
Maamuzi ya kuongeza bei ya mkate kwa serikali ya Sudan ni sehemu ya kufuata matakwa ya IMF ili kukuza uchumi wa nchi hiyo.