Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Licha ya uchumi mbaya,Sudan Kusini yatumia 'drones'
Sudani Kusini imeanzisha matumizi ya Kamera za usalama pamoja na ndege ndogo zisizo na rubani yaani'drones' ili kupambana na uhalifu katika mji mkuu Juba.
Viongozi katika nchi hiyo iliyoyumba kifedha wanasema wametumia mamilioni ya dola katika mradi huo. Mitambo hiyo itaongozwa na kampuni ya Israeli mpaka hapo wasudani wenyewe watakapoelimishwa jinsi ya kuitumia.
Sudani Kusini iliyopata uhuru miaka sita iliyopita imekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa miaka minne iliyopita. Huku viongozi wa serikali mara kwa mara wanalaumiwa kwa rushwa.