Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uwanja mkuu wa ndege Zimbabwe wapewa jina la Rais Robert Mugabe
Uwanja mkuu wa ndege nchini Zimbabwe umebadilishwa jina na kupewa rasmi jina la Rais Robert Mugabe.
Uwanja wa Kimataifa wa Harare sasa utaitwa uwanja wa Kimataifa wa Robert Mugabe.
Mtandao mmoja wa habari ulichapisha picha za sherehe hizo zilizofanyika mji mkuu Harare.
Barua kutoka kwa mamlaka za safari za ndege nchini humo kushauri kuhusu mabadiliko hayo ilisambatwa pakubwa kwenye mtandao wa Twitter mwezi Septemba
Mugabe, 93, ameitawala nchi hiyo tangu mwaka 1980.