Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Iran: Tutaunda silaha yoyote kujilinda
Rais wa Iran amesema kuwa nchi yake itaunda silaha zozote inazohitaji kujilinda dhidi ya uvamizi.
Wakati akihubia bunge Rais Hassan Rouhani, alisema kuwa Iran haitakuwa ikikiuka makubaliano yoyote ya kimataifa kwa kuunda silaha yakiwemo makombora ya masafa marefu.
Aliionya Marekani kuwa ukiukaji wa mkataba wa nyuklia uliotiwa sahihi kati ya Iran na mataifa sita yenye nguvu ni kwa manufaa yake.
Rais wa Marekani Donald Trump hivi karibuni alikataa kuidhinisha mkataba huo akiitaja Iran kama nchi kaidi inayounga mkono ugaidi.