Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rais mpya nchini Angola ameapishwa
Rais mpya wa Angola ameapishwa katika sherehe zilizofanyika kwenye mji mkuu Luanda.
Joao Lourenco alikula kiapo baada ya chama tawala cha MPLA kushinda uchaguzi.
Bw. Lourenco, ambaye ni waziri wa zamani wa usalama anachukua mahala pa Jose Eduardo Dos Santos, ambaye aliondoka madarakani baada ya kuiongzoa nchi kwa miaka 38.
Bwana Dos Santos atakuwa na ushawishi kwenye chama akiwa na haki ya kumteua mkuu wa polisi pamoja na mkuu wa majeshi.
Wakosoaji wanasema watoto wake, akiwemeo mwanamke tajiri zaidi barani Afrika, Isabel Dos Santos wamepewa nyadhifa za kudhibiti uchumi.
Licha ya Angola kuwa na utajiri wa mafuta, bado kuna mwanya mkubwa
Chama cha MPLA kimeitawala Angola tangu ipate uhuru wake kutoka Ureno mwaka 1975.