Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wapinzani Venezuela matatani
Bunge jipya la Katiba nchini Venezuela limepiga kura kwa kauli moja kuunga mkono viongozi wa upinzani kushtakiwa kwa makosa ya uhaini, kwa tuhuma za kuchochea nchi hiyo ikawekewa vikwazo vya kiuchumi na Marekani.
Agizo hilo linaelezea mashtaka hayo ni ya kihistoria na kusema kuwa wanakusudia kuwashugulikia wale wote wanaokwenda kinyume na matakwa ya raia wa kawaida wa Venezuela.
Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro mara kwa mara amekuwa akiwatuhumu viongozi wa upinzani kuwa upande wa Marekani, nchi ambayo anasema inajiandaa na uvamizi wa kijeshi.
Wiki iliyopita Rais Donald Trump aliamuru vikwazo vipya kwa Venezuela.