Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ndege iliowabeba waandishi wa habari yaanguka Kenya
Ndege ndogo iliokuwa ikiwabeba waandishi habari ilianguka muda mfupi baada ya kupaa katika uwanja wa ndege wa Wilson Airport mjini Nairobi kulingana na gazeti la Daily Nation.
Ndege hiyo aina ya Cessn ilikuwa imewabeba maripoa wawili na mpiga pich mmoja kutoka kituo cha ruminga ya Citizen ambao walikuwa wanaelekea kuchukua habari za muungano wa Upinzani Nasa katika eneo la Baringo.
Waandishi hao na wafanyikazi wa ndege hiyo wamepelekwa katika hospitali ya nairobi na wanadaiwa kuwa katika hali nzuri .
Gazeti hilo linasema kuwa kamanda wa polisi wa kitengo cha anagni Rodgers Mbithi alithibitisha ajali hiyo.