Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu 9 wauwawa katika mpaka wa Somalia na Kenya
Kumekuwa na shambulio jengine kusini mwa Kenya karibu na mpaka wa Somalia, ambapo takriban watu tisa wameuawa.
Baadhi ya ripoti zinasema waliouawa wote ni raia, kwa risasi na baadhi kwa mapanga.
Eneo hilo katika kaunti ya Lamu limeshuhudia mashambulio kadhaa ambapo polisi wanaamini yamefanywa na kundi la al Shabaab kutoka Somalia.
Kundi hilo pia limelenga majeshi ya Kenya yenye vituo vyao hapo kama sehemu ya jeshi la Umoja wa Afrika.