Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kangaroo afariki katika kiti akiwa na mvinyo Australia
Maafisa wa polisi wanachunguza baada ya kangaroo kupatikana amepigwa risasi huku akishikilia mvinyo wa pombe mjini Melbourne Australia.
Maafisa wa wanyama pori nchini Australia wanasema mnyama huyo aliigwa risasi mara tatu na baadaye kufungwa akiwa ameketi katika kiti.
Iliripotiwa mwezi uliopita lakini mamlaka ilitoa picha wiki hii katika harakati za kutafuta habari.
Hukumu ya mauaji ya myama huyo kinyume cha sheria ni faini ya hadi dola 36,500 za Australia na hadi kifungo cha miaka miwili jela.
Idara ya mazingira, ardhi, maji na mipango ilisema kuwa inashirikiana na maafisa wa polisi kutatua uhalifu huo.
Lazima ilichukua muda mrefu kumuweka kangaroo huyo katika hali aliyokuwa kanda kando ya barabara.
Hesabu ya hivi karibuni ya kangaroo nchini Australia ni milioni 34.3