Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Jaji afungwa kwa kukaidi agizo la mahakama India
Jaji mmoja nchini India ambaye amekuwa mafichoni tangu ahukumiwe kifungo jela amekamatwa na kufungwa.
Jaji CS Karnan alikuwa jaji wa kwanza wa mahakama kuu nchini India kukabiliwa na kifungo.
Alikamatwa katika jimbo la kusini la India Tamil Nadu siku ya Jumanne usiku.
Alihukumiwa kifungo mjini Kolkata huku ombi lake la kumwachilia kwa dhamana siku ya Jumatano likikataliwa na mahakamu ya juu zaidi .
Jaji huyo wa zamani alipatikana na hatia ya kutoa madai dhidi ya majaji wenzake.
Alihukumiwa kwa kukaidi agizi la mahakama na mahakama ya juu zaidi baada ya kutuma barua kwa waziri mkuu Narendra Modi ambapo alimtaka kuwachukulia hatua majaji wenzake.
Alipokonywa nguvu zake kama jaji mnamo mwezi Februari.