Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Faru amuua mtunza mazingira Rwanda
Mtunza mmoja wa mazingira ambaye alikuwa akisadia kuwapeleka Faru nchini Rwanda ameuawa na mmoja wa wanyama hao.
Shirika lililoandaa shughuli hiyo la African Parks, lilisema kuwa Krisztian Gyongyi, aliuwawa na Faru, katika mbuga ya taifa ya Akagera alipokuwa akiwafuatilia Faru hao.
Lakini taarifa hiyo haijasema kwa kina jinsi aliuwawa.
Mkurugenzi wa Shrika la Africa Parks Peter Fearnhead, alisema kuwa bwana Gyongyi alikuwa mtu muhimu kawarejesha Faru hao weusi na alikuwa eneo hilo kuwapa mafunzo walinzi wa mbuga jinsi ya kuwafuatilia na kuwalinda Faru
Faru hao walisafirishwa kutoka Afrika Kusini kuenda Rwanda mwezi uliopita.