Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Muwindaji alaliwa na kuuwawa na ndovu Zimbabwe
Mtaalamu mmoja wa uwindaji ameuwawa baada ya kulaliwa na ndovu ambaye alikuwa amepigwa risasi
Mtandao wa anaripotiwa kupigwa risasi wakati alimuinua Theunis Botha akitumia pembe yake kabla ya kuanguka na kufariki huku akimlalia na kumuaa bwana Botha.
Amekuwa akiongoza kundi la wawindaji karibu na mbuga ya Hwange nchini Zimbabwe wakati alifariki.
Mbuga hiyi ndiko simbna Cecil aliuwawa na muwindaji mmarekani mwezi Julai mwaka 2015 na kuzua shutuma kote duniani.
Bwana Botha an umri wa miaka 51 na baba wa watoto watano kutoka mkoa wa Limpopo nchini Afrika Kusini.
Mtandao wa Botha unasema kuwa alikuwa na ujuzi wa kuwinda Simba na Chui.
Vyombo vya habari nchini Afrika Kusini vilisema kuwa bwana Botha alikuwa rafiki wa muwindaji mwingine Van Zyl, ambaye mabaki yake yalipatikana ndani ya mamba mwezi uliopita.