Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanajeshi wa Kenya wawaua wapiganaji 50 wa al-Shabab
Jeshi la Kenya linasema kuwa limewaua zaidi ya wapiganaji 50 wa Al-Shaabab katika oparesheni iliyofanywa Kusini mwa Somalia.
Jeshi hilo lilisema lilinasa shehena ya silaha na risasi na kuharibu kabisa kambi ya wapiganaji hao katika eneo la Badhaadhe katika Lower Juba.
Hadi sasa Al Shaabab hawajasema lolote.
Maelfu ya wanajeshi wa Kenya wanahudumia nchini Somalia chini ya mwavuli wa Muungano wa Afrika.
Al Shaabab hufanya mashambulizi ya mara kwa mara kwenye mpaka na Kenya na pia kwenye kambi za wanajeshi wa Kenya walioko Somalia.