Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Diamond Platinumz azindua manukato Tanzania
Mwanamuziki mashuhuri nchini Tanzania Diamond Platinumz amepiga hatua nyingine baada ya kujitosa katika biashara ya uuzaji wa manukato.
Manukato ya mwanamuziki huyo yamepewa jina Chibu Perfume, kwa kufuata jina lake ya utani la Chibu Dangote.
Chupa ya manukato hayo inauzwa takriban Sh105,000 za Tanzania.
Diamond anaonekana kuwafuata wasanii wengine mashuhuri duniani ambao wamejiingiza katika biashara ya manukato na hutumia umaarufu wa nembo zao kujipatia mapato zaidi.