Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tathimini ya uharibifu wa kimbunga Debbie yaanza kufanyika Australia
Maofisa katika jimbo la Queensland nchini Australia wameanza kufanya tathimin ya madhara makubwa yaliyosababishwa na kimbuka Debbie, huku baadhi ya maeneo yakiwa hayawezi kufikiwa kutokana na barabara kuharibika na kujifunga kabisa.
Baadhi raia wameuelezea mji wa Bowen kwamba umeharibika na kuwa kama ukanda wa vita kutokana na kubomoka kwa majengo na mashamba ya ndizi.
Waziri mkuu wa Australia Malcolm Turnbull, amesema kuwa serikali imejiandaa vyema kukabiliana na madhara ya kimbunga hicho kilichoyakumba maeneo hayo.
Hata hivyo mamlaka nchini Austarilia zimeonya kuwa eneo la Pwani ya kaskazini mashariki nchini humo lililopo kilomita 1300 linatarajiwa kukumbwa na mafuriko ikiwa ni matokeo ya kimbunga hicho