Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Malaysia yaishutumu Korea Kaskazini kukiuka sheria za kimataifa
Waziri mkuu wa Malysia, Najib Razak ameishutumu Korea kaskazini kwa kukiuka sheria za kimataifa baada ya Pyongyang kuzuia raia wa Malaysia kuondoka nchini humo.
Bwana Najib naye haraka aliwazuia raia wa Korea kaskazini kuondoka nchini Malaysia.
Msuguano huu wa kidiplomasia umekuja kutokana na uchunguzi ambao Malaysia unaufanya kuhusu kifo cha kaka wa kambo wa Kiongozi wa Korea kaskazini kim jong Nam, aliyeuawa mjini Kuala lumpur mwezi uliopita.
waziri Razak amesema atafanya kila liwezekanalo kuwalinda raia wa Malaysia
Tangazo hilo limetolewa wakati Polisi wa Malaysia wakisema kuwa raia wawili wa Korea kaskazini wanatafutwa wakihusishwa na mauaji ya dhidi ya Kim jong nam na kuwa wamejificha kwenye ubalozi wa nchi yao mjini Kuala Lumpur.
Khalid Abubakar ni mkuu wa jeshi la Polisi nchini Malaysia
Mkuu huyo wa polisi amerejea kushutumu raia wa Korea kaskazini kutotoa ushirikiano kwa Polisi wanaofanya uchunguzi