Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wabunge wa Tanzania na Kenya wavamiwa Afrika Kusini
Wabunge wa bunge la Afrika kutokea mataifa ya Tanzania ,Kenya na Msumbiji walivamiwa na majambazi walipokua wakitoka uwanja wa ndege wa OR Tambo mjini Johannesburg wakielekea hotelini .
Mmoja ya wabunge hao kutokea Kenya alipigwa vibaya na majambazi hao alipokua akijaribu kuzozana nao wasiwaibie .
Wabunge wengi wanasema wakati umefika sasa bunge hilo la Afrika kuhamishwa kutoka Afrika Kusini kwa sababu hakuna usalama wa kutosha nchini humo.