Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mkufunzi wa Barcelona kubwaga manyanga
Mkufunzi wa klabu ya Barcelona Luis Enrique ametangaza kwamba atabwaga manyanga mwishoni mwa msimu huu.
Enrique atakuwa amehudumu kama meneja wa klabu hiyo kwa misimu mitatu .
Aliishindia klabu hiyo kombe la vilabu bingwa na mataji mengine mawili alipojiunga na Barcelona na kuwasaidia kushinda makombe 2 mwaka uliopita.
Lakini licha ya klabu hiyo kuongoa katika jedwali la ligi Barcelona iko katika hatari ya kubanduliwa katika kombe la vilabu bingwa Ulaya msimu huu baada ya kufungwa 4-0 na Prais St-Germain.
Enrique amesema kuwa sababu kuu ya yeye kutaka kujiuzulu ni kwamba anahitaji kupumzika.