Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
CIA kuchunguza iwapo Urusi ilingilia uchaguzi wa Marekani
Mwenyekiti wa kamati ya ujasusi katika bunge la Congress ambaye ni mwanachama wa Republican, Devin Nunes amesema wanachunguza ikiwa kulikua na ushirikiano wa kina kati ya Urusi na baadhi ya raia wa Marekani.
Taarifa hii inamaanisha kwamba suala la mchango wa Urusi katika uchaguzi wa Marekani linaendelea kutiliwa manaani.
Kamati ya ujasusi katika baraza la Congress imekua ikiichunguza Urusi kwa miaka mingi na wakati huu inalenga kubaini ikiwa kulikua na shughuli zozote za Urusi katika uchaguzi wa Marekani .
Tayari Idara ya FBI inachunguza muingilio wa Urusi katika uchaguzi wa Marekani.
Shirika la Ujasusi CIA na imekiri kwamba utawala wa Vladimr Putin ulinuia kusaidia Donald Trump kumharibia sifa mpinzani wake Hillary Clinton.
Donald Trump na timu yake wamekanusha kuwa baadhi ya watu kwenye timu ya Trump waliwasiliana na maafisa wa Urusi kabla ya Uchaguzi Mkuu.