Zaidi ya nyangumi 200 waliokwama ufuoni New Zealand warudi baharini

Watu wa kujitolea wamekuwa wakiwasaidia nyangumi waliokwama kwenye ufuo huo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Watu wa kujitolea wamekuwa wakiwasaidia nyangumi waliokwama kwenye ufuo huo

Wanamazingira nchini New Zealand, wanasema zaidi ya nyangumi 200 waliokuwa wamekwama ufuoni sasa wamemudu kurudi wenyewe maji makuu.

Hata hivyo bado kuna wengine 17 ambao wangali wamekwama ufuoni na sasa wanatunzwa hadi pale mawimbi yatakapokuwa makubwa ili wasaidiwe kurudi baharini.

Eneo hilo la pwani la kilomita 20, lenye maji ya kina kifupi, ni gumu kwa nyangumi kuogelea.

Watu wa kujitolea wamekuwa wakiwasaidia nyangumi waliokwama kwenye ufuo huo

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Watu wa kujitolea wamekuwa wakiwasaidia nyangumi waliokwama kwenye ufuo huo

Jana maafisa na watu wa kujitolea walisaidia kundi lingine la nyangumi karibu 100 waliokwama kwenye ufuo huohuo wa Farewell Spit huko New Zealand.

Nyangumi hao walikuwa ni sehemu ya wale 400 waliokwama baharini juzi huku waliosalia 300 wakifariki, katika kisa ambacho kinatajwa kuwa kibaya zaidi kuwahi kutokea nchini humo.

A volunteer tends to a whale as they prepare to refloat them after one of the country's largest recorded mass whale strandings, in Golden Bay, at the top of New Zealand's South Island, 12 February 2017

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Volunteers tend to the latest pod of whales to arrive on New Zealand's South Island

Bado wanasayansi hawajafanikiwa kufahamu ni kwa nini nyangumi hufika kwenye ufuo wa bahari.

Lakini inadhaniwa huwa inatokea kwa sababu nyangumi huzeeka , huugua au huwa wameumia na kupoteza mwelekeo.

Wakati mwingine, nyangumi anapokwama baharini, huwalilia wenzake ambao watafika kujaribu kumuokoa lakini kisha nao wanajipata wamekwama.

Nyangumi waliokwama New Zealand

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Nyangumi waliokwama New Zealand
Golden Bay, New Zealand
Maelezo ya picha, Golden Bay, New Zealand