Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Amri ya kutotembea yatangazwa Mogadishu
Maeneo kadha ya mji mkuu wa Somalia Magadishu yamewekwa chini ya amri ya kutotembea, siku moja kabla ya wabunge wa kumchagua rais mpya.
Hatua hizo za kiusalama zinalenga maeneo yanayozunguka uwanja wa ndege eneo ambalo kura itafanyika, licha ya wasiwasi wa kuwa huenda kukatokea shambulizi kutoka kwa wanamgambo wa kiislamu wa al Shabab.
Marufuku ya safari za ndege kupitia maeneo fulani nayo imetangazwa. Somalia haijakuwa na serikala kamili tangu utawala wa Siad Barre uanguke mwaka 1991.