Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mkewe El Chapo akatazwa kumuona mumewe
Mlanguzi mkuu wa madawa ya kulevya, raia wa Mexico, Joaquin Guzman, amelalamika alipofikishwa mahakamani mjini New York, akisema kuwa anazuiliwa kwa njia isiyofaa katika gereza moja la Marekani.
Guzman, ambaye amefanikiwa kutoroka mara mbili kutoka magereza ya Mexico, aliwahi kutoroka kupitia kikapu kikubwa na mara ya pili alichimba shimo kubwa chini ya ardhi kupitia seli yake. Hivi sasa anazuiliwa akiwa pekee katika gereza lenye ulinzi mkali jijini New York.
Mawakili wake wanasema kuwa mkewe amezuiliwa kumtembelea tangu asafirishwe chini ya ulinzi mkali kutoka Mexico mwezi uliopita.
Wakati mwingi Guzman haruhusiwi kutangamana na wafungwa wengine.
Guzman anashtakiwa kwa kuwa na silaha kinyume cha sheria ya ulagunzi wa madawa ya kulevya.