Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Walio na akili punguani kupokonywa bunduki Marekani
Bunge la uwakilishi nchini Marekani limepiga kura kuondoa sheria inayowaruhusu watu walio na akili punguani kumiliki bunduki.
Chini ya sheria hiyo iliopitishwa na utawala wa Barrack Obama uchunguzi wa kina utafanyiwa mtu anayetarajiwa kumiliki bunduki hiyo ambaye hupata ufadhili wa walemavu na ana matatizo ya kiakili.
Mwenyekiti wa kamati ya haki Bob Goodlatte amesema kuwa sheria hiyo inabagua na kwamba hakuna ushahidi wowote kwamba watu walio na akili punguani wako hatarini mbele ya umma.
Rais Donald Trump alifanya kampeni na kuahidi kwamba Wamarekani wataendelea kumiliki bunduki.