Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Israel kujenga makaazi 3000 zaidi huko West Bank
Taifa la Israel limetengaza mipango ya kujenga makaazi 3000 zaidi katika ene la West Bank .
Hatua hiyo inajiri baada ya serikali kuidhinisha ujenzi wa nyumba 2500 na nyengine 100 zaidi mashariki mwa Jerusalem.
Wapalestina wanadai umiliki wa maeneo yote mawili.
Awali jeshi la Israel lilikuwa linajiandaa kutekeleza operesheni ya agizo la mahakama ya kuwandoa walowezi waliojenga katika eneo la Amona katika eneo la West bank.
Siku ya Jumatatu wakaazi walipewa makataa ya saa 48 kuondoka.
Walowezi hao waliokuwa wamejenga katika ardhi ya Palestina .