Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mkuu wa magereza akamatwa akitoroka Gambia
Maafisi wa polisi nchini Senegal wanasema kuwa wamemkamata mkuu wa magereza nchini Gambia Jenerali Bora Colley alipojaribu kuvuka na kuelekea Guinea Bissau.
Taarifa ya polisi inasema kuwa alikamatwa siku ya Jumatano na baadaye kukabidhiwa jeshi la Senegal.
Makundi ya haki za kibinaadamu yanasema kuwa kiwango kikubwa cha ukandamizi ulifanywa chini ya uongozi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh ikiwemo mateso pamoja na mauaji ya kiholela ambayo yalifanyika katika jela.
Senegal ilichukua jukumu muhimu la kumsihi rais Yahya Jammeh kuondoka nchini humo siku ya Jumamosi.