Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wabukala aidhinishwa kuwa mwenyekiti wa tume ya kupambana na rushwa Kenya
Askofu mstaafu wa kanisa la kianglikana nchini Kenya Eliud Wabukala, ndiye mwenyekiti mpya wa tume ya kupambana na ruswa nchini Kenya(EACC)
Uteuzi wa bwana Wabukala na Rais Uhuru Kenya uliidhinishwa na bunge Jumanne jioni.
Anachukua mahala pa Philip Kinisu, ambaye aliondolewa ofisini baada ya kutajwa kwenye kashfa ambayo ilikumba idara ya huduma kwa vijana.
Wakati wa kikao maalum cha bunge, wabunge waliunga mkono kwa wingi uteuzi wa Wabukala, wakiwa na matumaini kuwa askofu huyo mstaafu atakabiliana na mitandao ya ufisadi nchini Kenya.
Kiongozi wa wengi katika bunge la Kenya Aden Duale, amesema kuwa Wabukala anaingia katika tume hatari ambayo ufisadi hujipigania na ambayo wanyeviti wengine sita wameondoka bila kutekeleza lolote la kukabiliana na ufisadi.