Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Donald Trump: Nitashirikiana na Urusi na China
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kushirikiana na Urusi na China, iwapo mataifa hayo yatashirikiana naye.
Katika mahojiano na Wall street journal, bw Trump amesema vikwazo vilivyowekewa Urusi hivi majuzi, vitaendelea kuwepo, japo huenda vikaondolewa iwapo Urusi itasaidia Marekani katika vita dhidi ya ugaidi.
Anatumai kwamba atakuwa na kikao na rais Putin hivi karibuni.
Pia amesema kuwa sera ya One China ambayo Marekani haitambui Taiwan itajadiliwa upya.
Wakati huohuo kamati ya bunge la seneti nchini Marekani imetangaza kwamba itachunguza madai kwamba urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani.