Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Pena Nieto amjibu Trump kuhusu Ukuta
Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto amesisitiza kwa mara nyengine kwamba nchi yake haitalipia ukuta katika mpaka na Marekani.
Ametoa kauli hiyo baada ya Rais mteule wa Marekani, Donald Trump kusema katika mkutano wake na waandishi wa habari kwamba anataka kuanza kuujenga haraka na kwamba Mexico itailipa Marekani kwa gharama iliyoingia.
Bwana Pena Nieto amewaambia wanadiplomasia wa kigeni kwamba yuko tayari kujadili mustakbali wa makubaliano ya kibiashara ya Kaskazini ya Marekani, ambapo Trump amesema hayo ni makubaliano mabaya ya kibiashara kuwahi kupitishwa na Marekani.