Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wakenya wamsuta Rais Kenyatta mtandaoni
Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakimsuta Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kufuatia hatua zake za kuzindua miradi.
Wakosoaji wanasema kuwa baadhi ya miradi ilizinduliwa na Rais Kenyatta ilikuwa ikiendelea au tayari ilikuwa imezinduliwa.
Wengine nao wanasema kuwa hatua hiyo iko chini ya hadhi ya rais.
Wiki iliyopita bwana Kenyatta ambaye atawania urais tena mwezi Agosti alikuwa mjini Mombasa ambape alizindua daraja.
Baadhi wa watumiaji wa mtandao wa Twitter wametumia uzinduzi huo kama chanzo cha kumsuta rais.
Wakitumia #UhuruChallenge, wamechapisha mifano yao ya vitu walikuwa wakizindua.
Maeneo kadha ukiwemo mji mkuu Nairobi, pwani na maeneo ya kaskazini mwa nchi yamekuwa yakikumbwa na ukoseu wa nguvu za umeme hali iliyosababisha rais kusutwa zaidi