Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Urusi na Marekani zalaani shambulio Uturuki
Nchi kadha zimelaani mashambulio hayo katika klabu ya starehe mjini Istanbul.
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, amesema ni shida kufikiria uhalifu mbaya zaidi, kushinda kuuwa raia wakati wanasherehekea mwaka mpya.
Ameahidi kuwa mshirika wa kuaminika wa Uturuki, katika mapambano yake dhidi ya ugaidi.
Nchini Marekani, Ikulu ililaani kile ilichokiita "ukatili wa shambulio la kigaidi".