Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Makubaliano ya kisiasa nchini DR Congo yakwama
Makubaliano ya kisiasa kati ya serikali na upinzani nchini DR Congo ili kumaliza mgogoro wa kisiasa yamekwama katika dakika ya mwisho.
Muhula wa rais Joseph Kabila ulikamilika mapema mwezi huu ,lakini uchaguzi umeahirishwa huku makumi ya watu wakipoteza maisha yao katika maandamano.
Wapatanishi kutoka kanisa Katoliki awali walikuwa wamesema kwamba pande hizo mbili zilikuwa zinakaribia maafikiano ambapo rais Kabila atasalia mamlakani hadi uchaguzi utakapoandaliwa mwishoni mwa 2017 .
Hatahivyo baadhi ya makubaliano hayakuafikiwa hivyobasi kuahirisha sherehe ya kutia kandarasi makubaliano hayo huku mazungumzo yakiendelea.