Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Misri yamkamata mwanahabari wa Al-Jazeera
Serikali ya Misri imedhibitisha kwamba inamzuilia mwanahabari kutoka shirika la habari la AlJazeera aliyekamatwa Ijumaa.
Wizara ya usalama wa ndani inasema mwanahabari huyo, Mahmoud Hussein, atazuiliwa kwa kipindi cha siku 15 kwa tuhuma za kuchochea maasi na kusambaza habari za uongo.
Al Jazeera imepigwa marufuku ya kuendesha shughuli zake nchini Misri, na imelaani hatua hiyo.
Kulingana na Aljazeera, mwanahabari huyo raia wa Misri alikuwa nchini humo likizoni.
Aljazeera inahofia usalama wa mwanahabari huyo.