Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wakosoaji wa Castro wafurahia kifo chake
Wakosoaji wa mwanamapinduzi, aliyekuwa kiongozi wa Cuba, Fidel Castro, wanaoishi Miami, nchini Marekani, kilomita 200 kutoka ufuo wa Bahari wa Cuba, walifanya maadhimisho ya hadharani kufuatia kutangazwa kwa kifo cha kiongozi huyo.
Wengi wao walihamia Miami baada ya Castro kupindua Serikali yenye ufisadi mkubwa, iliyokuwa ikiungwa mkono na Marekani mwaka 1959.
Wengine wengi waliungana nao baada ya muungano wa Sovieti, taifa lililokuwa likifadhili Cuba, kusambaratika na kusababisha mfumuko mkubwa wa bei.
Wakaazi wengi waliokumbuka umaskini na mateso ya kisiasa na kidini aliyokuwa akiwalimbikizia Castro, wengi waliendesha magari yao wakipiga honi kwa shangwe
Wengi walisikika wakipiga makelelewa wakisema Cuba sio Castro No!.